Skip to main content

KUMBUKUMBU YA KIFO CHA SOKONE



WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Watanzania wana mengi ya kujifunza kutoka aliyekuwa Waziri Mkuu wa tatu wa Tanzania, hayati Edward Moringe Sokoine kwa jinsi alivyokuwa kielelezo cha utumishi wa watu na kielelezo cha kupigania wanyonge.Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Aprili 12, 2011) wakati akitoa salamu za Serikali katika ibada ya kumbukumbu ya miaka 27 ya kifo cha hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mt. Paulo wa Msalaba mjini Dodoma.
“Marehemu Sokoine atakumbukwa kwa mengi ambayo kwa kweli tukiyaongelea hapa hatutayamaliza; ninachoweza kusema, leo tunamkumbuka mtu ambaye kwetu sisi Watanzania, ni kielelezo bora cha utumishi wa watu, kielelezo cha kujituma, kielelezo cha upendo, kielelelzo cha kupenda haki kielelezo cha kupigania wanyonge na kielelezo cha kumcha na kumtumikia Mungu,” alisema.

Alisema katika utumishi wake, Mzee Sokoine alifanya bidii kutetea wanyonge na maslahi yao kwa kupambana na watu wanaohodhi bidhaa (walanguzi na wahujumu uchumi) hadi wakasalimu amri. “Wakati akitangaza vita dhidi ya walanguzi, nakumbuka alitoa kauli hii: Kama wanasema Serikali ilikuwa likizo, sasa wajue kuwa likizo imekwisha,” alisema Waziri Mkuu akimnukuu hayati Sokoine.“Alitumia muda mwingi kujenga jamii inayochukia rushwa na ulanguzi... Japo hayupo kati yetu kimwili, faraja ninayoipata mimi kama Pinda, tunapoadhimisha kumbukumbu kama hii ni kuwa bado huyu mwenzetu tuko naye kimawazo, kiakili na kubwa zaidi kiroho,” alisema.

Mkuu alisema marehemu Sokoine alikuwa kiongozi wa kipekee kwani aliamini kwamba, kuwajibika kama kiongozi ni kukubali kwa hiari dhamana ya uongozi unayopewa ama kwa njia ya kuomba kwa kura au kwa kuteuliwa Kikatiba au Kisheria. “Aliamini kuwa Kiongozi lazima akubali kutumia dhamana ya uongozi aliopewa kwa maslahi ya umma na kwa Taifa kwa ujumla.”

Waziri Mkuu Pinda alisema: “Marehemu Sokoine amefanya mengi mazuri ambayo tunayakumbuka leo. Hebu tujifunze kutoka kwake kwamba; mazuri tunayoyafanya leo, huwa furaha ya kesho. Tumuige kwa kufanya mazuri ambayo yatakumbukwa daima na vizazi vijavyo,” alisema.
“Marehemu Sokoine alikuwa muasisi wa biashara huria nchini wakati tukiwa kwenye itikadi ya Ujamaa. Aidha, alikuwa na wazo zuri la kuanzisha usafiri wa daladala Dar es Salaam. Wakati wake mabasi makubwa ya ofisini yalitumika kubeba watu Jijini Dar es Salaam na hii ni kielelezo cha kuujali umma wa Watanzania,” alisema.

Mapema akitoa mahubiri katika ibada hiyo, Askofu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Mhashamu Askofu Gervas John Nyaisonga alisema kumbukumbu ya kifo cha Sokoine iwakumbushe Watanzania ni nini cha kujifunza kutoka kwake kuenzi tunu alizoacha.
Alisema alikuwa mtu wa kipekee kwani alijitolea kukatwa asilimia 50 ya mshahara wake ili kuchangia katika mfuko wa nguvukazi ili wananchi wasio na uwezo wa kukopa benki waweze kupata mikopo kutoka katika mfuko huo.

Ibada hiyo iliyoongozwa na Askofu Nyaisonga kwa kushirikiana na mapadri wengine saba ilihudhuriwa na wanafamilia wa Sokoine, Spika wa Bunge, Bibi Anna Makinda, Waziri Mkuu mstaafu, Bw. Edward Lowassa, Wabunge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, wakuu wa wilaya na waumini mbalimbali kutoka Dodoma, Mvomero na Arusha.
Edward Moringe Sokine ambaye alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 46, aliwahi kuwa Waziri Mkuu kwa vipindi viwili cha kwanza kikiwa ni Februari 13, 1977 hadi Novemba 7, 1980 na kipindi cha pili kuanzia Februari 23, 1983 hadi Aprili 12, 1984 alipofariki kwa ajali ya gari Wami Dakawa, mkoani Morogoro akiwa njiani kurejea Dar es Salaam kutoka Dodoma ambako alikuwa akihudhuria mkutano wa Bunge.
IMETOLEWA NA:OFISI YA WAZIRI MKUU,S. L. P. 980,DODOMA.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...